James Munisi
James Munisi

@NjiwaFLow

20 Tweets 2 reads Dec 08, 2022
MFAHAMU ‘Bruce Reynolds’ MASTERMIND WA TUKIO LA ‘Great Train Robbery’.
SEHEMU YA PILI
#UZI
💨Saa 18:50, Jumatano ya Tar 7 Aug Mwaka 1963, Royal Mail train ilikua imepaki pale Glasgow Central station, tayari kwa ajili ya kuanza safari ya kuitafuta Euston Station iliyoko London
Treni hio ilikua ikitarajiwa kufika
Euston Station, saa kumi alfajiri ya siku iliyofuata.
Treni hio ilikua na mabehewa 12, na ndani yake kulikuwa na Post Office staff kama 72, ambao hao kazi yao ilikua ni ‘Ku-sort mail during the journey’.
Miongoni mwa mabehewa hayo, kulikuwa na behewa moja ambalo lilikuwa limesheheni maburungutu ya fedha, ikikadiliwa value ya shipment ilikuwa kama £300,000, ila Kwasababu Weekend iliyopita kulikua na kile kinachofahamika kama ‘UK Bank Holiday’,
hiyo kupelekea kiasi cha fedha..
…ambacho kilikua kikisafirishwa siku hile kukadiliwa kufikia kati ya £2.5 mpaka £3 million.
Nyuma kidogo, Mwaka 1960 Post Office Investigation Branch (IB), wali recommend kuwepo kwa alarms kwenye ofisi zote za posta zilizopo kwenye vyombo vya usafiri kama treni…..
..yaani Travelling post office (TPO),hususani kwenye mabehewa yanayobeba mizigo yenye thamani kubwa, HVP (high-value packages)
Hio recommendation ikafanyiwa kazi mwaka 1961, na mabehewa yote ya HVP ambayo hayakufungwa mifumo ya alarm yaliwekwa kwenye kama reserve kwenye karakana
Mwaka 1963, mabehewa yale kadhaa yaliyokuwa hayajafungwa mifumo ya HVP yalifungwa mifumo hio na kisha yakajumuishwa siku hio ya safari, isipokuwa hakukuwa na Mzigo wowote wa thamani ambao uliwekwa kwenye mabehewa hayo.
Saa 03:00 ya usiku wa August 8 ya mwaka huo wa 1963, aliyejifanya kama dereva wa treni hio aliyekuwa akifahamika kama Mzee Jack Mills, ambaye alikuwa na umri wa miaka 58, alisimamisha treni hio pale West Coast Main Line baada ya kuona alama ya taa nyekundu katika mbele yake.
Hapo ilikua ni kwenye railway crossing ya kati ya Leighton Buzzard na Cheddington.
Kuwashwa kwa taa hio, ilikuwa ni ishara tosha kuwa, Bruce na kundi lake walikuwa wakiianza kazi rasmi mida hiyo ya wanga
Baadhi ya Wezi hao tayari walikuwa wameshazama ndani ya treni, na kisha walichokuwa wakikiwaza sasa ni kuchukua maburungutu ya fedha yaliyokuwamo humo.
Wakaichukua treni hiyo na kisha ikaendeshwa mpaka eneo linalofahamika kama Bridego Bridge (Kwa sasa Mentmore Bridge).
Siku ya tukio, Bruce na wenzake waliajiri mtu mwingine ambaye naye pia alikuwa na uzoefu wa kuendesha treni aitwaye Ronnie Biggs, isipokuwa Ronnie yeye alikuwa hana uzoefu sana na mifumo mipya ya engine za treni na by the way yeye alikuwa amesha staafu kazi hio.
Hivyo kazi ya uendeshwaji wa treni bado ikabaki kwa Mills, na huku Ronnie yeye akapewa kitengo kingine cha kwenda kwenye gari iliyokuwa ikiwasubiri ili akasaidie kupakua Mzigo baada ya kuifikisha treni hapo.
Treni ikawasili pale Bridego Bridge chini ya dereva, Mills.
Kundi la pili la kina Bruce halikuwa na kazi nyingine zaidi ya kuvamia ya mabehewa yaliyokuwa yamesheheni maburungutu ya fedha.
Kulikua na kakundi kengine kadogo, chini ya Frank Dewhurst, ambao hawa walipewa kazi Maalumu na Bruce ya kuhakikisha wana wadhibti wale wafanyakazi watatu wa treni waliokuwamo kwenye zile ofisi za posta zilizokuwamo mle ndani ya Treni, ambao walikuwa ni L Penn, J Ware na O'Connor
Mabehewani Kulikuwamo na watu kadhaa ambao walijaribu kuwazuia wale wezi bila mafanikio.
Waliamuriwa walale chini, wakatiwa pingu, na kisha wezi wakaanza kufanya kile walichokijia.
Baada ya dk 20-25, kina Bruce walikuwa wamefanikiwa kuchukua kila walichokuwa wamekijia, na kisha kwa gari zao mbili aina ya Land Rover ambazo zote zilikuwa na registration plates BMG 757A, wakaondoka eneo la tukio kwa haraka sana.
Safari yao ilikua ni kwa njia zisizo rasmi, na ndani ya gari zote mbili walikuwa wakisikiliza redio ili kujua kama kuna taarifa zozote za kiusalama ambazo polisi wangekuwa wanazitangaza juu ya tukio lao.
Wakawasili Leatherslade Farm, Mida ya saa 4:30 alafajiri,…
…muda huo ndio kwa mara ya kwanza wakasikia vyombo vya habari vikitangaza juu ya tukio hilo.
Hapo Leatherslade Farm, hapo wakavigawa vibunda katika mabegi madogo madogo, na kisha kupitia redio, wakajua kuwa polisi waliwasanukia kuwa hawakuwa mbali sana na eneo la tukio.
Hilo shamba lilikua kama 50KM kutoka eneo la tukio, na kwakutumia gari linalokimbia vizuri, wakajua Polisi wangeweza kufika hapo kwa kutumia kama dk 30 tu.
Tukio hilo lilitokea Alhamis, na walikuwa na plan ya kuondoka shambani hapo, jumapili ila baada ya hesabu hizo wakaona…
… hapana, wataondoka hapo Ijumaa ili kuwapa mda mfupi wa polisi kuwachunguza na kuwapata.
Pia wakasanuka kuwa endapo kama watatumia magari yale yale ya Land Rover, wangeweza kushtukiwa na baadhi ya mashuhuda ambao walikuwa mle mabehewani kwani waliwaona na gari hizo.
Vipi sasa, walifanikiwa kutoboa!!?
Endelea Kufuatilia kisa hiki, hapa hapa.
Tukutane Kesho, Muda na Wakati kama huu🙃

Loading suggestions...