Deograsius Andrew๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ
Deograsius Andrew๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

@Deodravis

10 tweets 58 reads Apr 25, 2023
NJIA TANO MUHIMU ZA KUIJENGA TABIA YA KUWEKA AKIBA.
UZI. (Muhimu)
Tafiti zinasema ni watu 14 tu kati ya watu 10,000 ndio wanatabia asili ya kuweka akiba na hao ndio wanaofanikiwa kirahisi. Sasa kama wewe unatatizo la kushindwa kuweka akiba kama mimi basi
Twende sawa.๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ
Kabla hatujaendelea nikuombe
kama bado hujanifollow basi nifollow sasa
@Deodravis @Deodravis @Deodravis
Nami nitakufollow back.
Tuendelee. ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ
Kila mtu huwa anatamani atimize malengo yake na njia pekee ya kuyafikia malengo ni kujiwekea akiba na kuwa na tabia ya kutotumia vibaya fedha hata kama ni chache toka kwenye kipato chako kidogo.
Leo nimekuletea njia Tano ambazo zimewasaidia wengi kujiwekea akiba na kufanikiwa ๐Ÿ‘‡๐Ÿฟ
1. JIWEKEE MAZOEA YA KUANDAA BAJETI YAKO NA UIZINGATIE
Hapa inabidi ujipe kipaumbele mwenyewe lakini ufuate vipengele hivi.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Orodhesha mapato yako yote ya pesa
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Ainisha matumizi yako na hakikisha unayabana ili upate baki.
Lakini cha muhimu zaidi hapa ni kuisimamia bajeti.
2. TAFUTA NJIA NZURI YA KUWEKA AKIBA YAKO.
Hapa namaanisha njia ambayo itakupa kizuizi cha kuzifikia hizo fedha kirahisi kama vile.:
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Kibubu chenye kufuri.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Fixed Account ya bank
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Kuzituma kwa mtu unaemuamini aliye mbali na wewe.
Hii itategemea na ipi unaipendelea.
3. YAJUE VEMA MATUMIZI YAKO NA HAKIKISHA UNAYASIMAMIA.
Hapa namaanisha.:
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Tambua matumizi gani unayafanya mara kwa mara
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Tambua matumiz ambayo hayaepukiki.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Tambua pia matumizi yasiyo ya lazima na uyaepuke kadri uwezavyo
Hapa utaongeza uwezo wako wa kuweka akiba.
4. WEKA AKIBA KIDOGO KIDOGO LAKINI MARA NYINGI UWEZAVYO.
Wazungu husema "Save little but often" hivyo.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Iwe elfu, mia iweke kwenye akiba.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Usiache chenji bar ama sokoni badala yake hiyo chenji ndiyo uihifadhi.
Hii itakurahisishia kutopoteza hela ndogo ndogo pia.
5. TATHIMINI AKIBA YAKO BAADA YA MUDA FULANI.
Baada ya kipindi kisichopungua miezi 6 fanya tathimini.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ kiasi gani umeweza kuweka kwa kipindi hicho.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ kiasi gani waweza kuweka kwa kipindi zaidi ya hicho.
๐Ÿ‘‰๐Ÿฟ Njia gani waweza zitumia kuongeza uwezo wako wa kuweka akiba.
NB: Najua yapo mengi sana lakini haya ndio ambayo yanajenga tabia ya kuweka akiba. Ingawa sio wote wanaopitia njia hizi za kujiwekea akiba kama nilivyosema mwanzo kwani wapo ambao kuweka akiba ni tabia yao ya kuzaliwa.
๐Ÿ™๐ŸฟMWISHO WA UZI. ๐Ÿ™๐Ÿฟ
Tafadhali RETWEET

Report this thread